DIAMOND NA NGASSA KWENYE PIPA...PLUTINUMZ AITAKIA KILA LA HERI STARS CHALLENGE
DIAMOND NA NGASSA KWENYE PIPA...PLUTINUMZ AITAKIA KILA LA HERI STARS CHALLENGE
 |
| Kila
la heri mwana; Mrisho Ngassa alikutana na Diamond Plutinumz jana jioni
kwenye Ndege wakati timu ya soka ya Tanzania Bara, Kilimanjaro Stars
ikisafiri kutoka Mombasa kwenda Nairobi, tayari kwa mchezo wa Nusu
Fainali Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge
dhidi ya wenyeji, Kenya Jumanne Uwanja wa Kenyatta, Machakos. Stars
ilicheza na Uganda juzi, The Cranes Uwanja wa County ya Mombasa, zamani
Manispaa na kuitoa kwa penalti 3-2 kufuatia sare ya 2-2 ndani ya dakika
90, wakati Diamond alifanya onyesho usiku wa siku hiyo ufukwe wa Big
Tree Resort, Mombasa na kupagawisha ile mbaya. Wawili hao ni marafiki na
wamewahi kufanya tangazo la biashara pamoja. Diamond alimtakia kila la
heri Ngassa na Stars katika mchezo wao wa Jumanne na akasema angeweza
kubaki, lakini tayari ana mikataba ya maonyesho mengine Dar es Salaam
kuanzia jana Coco Beach. |
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni