JOSE Mourinho ameweka wazi kuwa kipa
namba moja wa muda mrefu wa Chelsea, Petr Cech anaweza kuondoka klabuni hapo
majira haya ya kiangazi mwaka huu.
Baada ya Thibaut Courtois kurejea
klabuni kutokea klabu ya Atletico Madrid alipokuwa anacheza kwa mkopo, tetesi
zimeshaanza kuzuka kama kipa wa kimataifa wa Jamhuri ya Czech ataendelea
kushikilia namba moja katika dimba la Stamford Bridge.
Mtandao wa Goal unafahamu
kuwa Chelsea wapo tayari kusikiliza ofa kutoka klabu ya PSG iliyoonesha nia ,
na Mourinho amesema Cech anaweza kuondoka kwa kutegemea Mark Schwarzer kuwa
kipa namba mbili.
“Petr yupo tayari kupigania nafasi
yake, lakini Thibaut ni kipa bora zaidi kijana duniani, hakuna wasiwasi juu ya
hilo,” Kocha huyo Mreno alikaririwa akizungumza na Evening Standard.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni