Tafuta katika Blogu Hii

Ijumaa, 1 Agosti 2014

BOSI WA CHELSEA JOSE MOURINHO AMTOA ‘KAFARA’ PETR CECH -



JOSE Mourinho ameweka wazi kuwa kipa namba moja wa muda mrefu wa Chelsea, Petr Cech anaweza kuondoka klabuni hapo majira haya ya kiangazi mwaka huu.
Baada ya Thibaut Courtois kurejea klabuni kutokea klabu ya Atletico Madrid alipokuwa anacheza kwa mkopo, tetesi zimeshaanza kuzuka kama kipa wa kimataifa wa Jamhuri ya Czech ataendelea kushikilia namba moja katika dimba la Stamford Bridge.
Mtandao wa Goal unafahamu kuwa Chelsea wapo tayari kusikiliza ofa kutoka klabu ya PSG iliyoonesha nia , na Mourinho amesema Cech anaweza kuondoka kwa kutegemea Mark Schwarzer kuwa kipa namba mbili.
“Petr yupo tayari kupigania nafasi yake, lakini Thibaut ni kipa bora zaidi kijana duniani, hakuna wasiwasi juu ya hilo,” Kocha huyo Mreno alikaririwa akizungumza na Evening Standard.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni